Baada ya kumponya yule mtu kilema kwenye bwawa la Bethzatha, Yesu aliwaambia viongozi wa kidini kwamba walikuwa na uthibitisho wa kutosha wa kumtambulisha kuwa Masihi aliyeahidiwa. Alisema Musa, Yohana Mbatizaji, ‘sauti ya Mungu’ kutoka mbinguni, na maandiko yote yaliunga mkono dai lake. Yesu alilisha zaidi ya watu 5,000 na kudai kuwa ni Mkate wa Uzima. Yesu alifundisha kwamba wale wanaokuja kwake wakiwa na nia ya kufanya yale anayosema watajua kwamba mafundisho yake yanatoka kwa Mungu.
Toa Jibu
Ni lazima uingie ndani kutuma maoni.