Mambo ya Walawi, ‘mwongozo huu wa ukuhani’, unaeleza jinsi shughuli zote za ukuhani wa Walawi zilivyokuwa zikiwafundisha watu wa Mungu kuhusu utakatifu na utakaso katika kumtumikia Bwana. Kiini cha kitabu hicho kinapatikana katika sura ya 11-22, ambapo “kutakaswa kwa watu wa Mungu” kunafafanuliwa. Hema la kukutania na makuhani waliohudumu hapo walikuwa ni tangazo la Mungu kwa ulimwengu wote kwamba watu waliochaguliwa na Mungu walikuwa watu watakatifu kwa sababu Mungu wao alikuwa mtakatifu.
Toa Jibu
Ni lazima uingie ndani kutuma maoni.