Malaki ndiye nabii wa mwisho katika Agano la Kale. Alihubiri baada ya wakati wa Nehemia, wakati watu wa Mungu walikuwa na namna ya dini lakini walikataa ukweli wa uhusiano wao na Mungu. Ujumbe wa moyo wake ulikuwa kwamba Mungu alitaka kuwa na uhusiano wa upendo na watu wake. Walifanya matambiko ambayo walifikiri Mungu alitaka, lakini walikuwa wamepoa kiroho na hawakujali. Malaki akawa mjumbe wa toba Mungu alimtumia kuwavuta watu wake warudi kwake.
Toa Jibu
Ni lazima uingie ndani kutuma maoni.