Hosea alikuwa nabii wa upendo wa Mungu kwa makabila kumi ya ufalme wa kaskazini wa Israeli wakati wa ufalme uliogawanyika. Watu wa Israeli walikuwa wamemwacha Mungu na kuabudu sanamu – uzinzi wa kiroho. Hosea alioa kahaba na kumpenda bila masharti kama wonyesho hai wa upendo wa Mungu_x0092. Kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wa Israeli, makabila hayo kumi hayangesikika tena, hata hivyo Hosea alitabiri kurudi kwao kiroho kwa Mungu siku moja.
Toa Jibu
Ni lazima uingie ndani kutuma maoni.