Tukimfuata Yesu na kuwa na mawazo yake, tutabadilishwa. Tutakuwa chumvi ya dunia na kama mianga inayomulika duniani. Hiyo ina maana kwamba hatutaishi jinsi wengine wanavyoishi. Tutafanya zaidi kwa sababu tunaye Yesu anayeishi ndani ya mioyo yetu. Tutakuwa na upendo mkuu kuliko ulimwengu unavyojua na kuonyesha neema na rehema kuu kuliko ulimwengu unavyoelewa. Kwa kufanya hivyo, tutakuwa kama Baba yetu wa mbinguni.
Toa Jibu
Ni lazima uingie ndani kutuma maoni.